Friday, 2 February 2024

MWANAFUNZI ALILIA JOHN MAKALI NA MAKABICHI

 

Mwanafunzi mmoja kwa jina Joseph Owino kutoka Musikoma eneobunge la Kanduyi kaunti ya Bungoma  amejiwasilisha katika shule ya wavulana ya Ndivisi   akiwa na barua yake pekee, bila mzazi, na vifaa muhimu vya masomo.

Joseph Owino 


Owino ambaye ni alipata alama 338  katika shule ya Moi Primary anasema juhudi zake za kupata msaada kutoka kwa eneobunge la CDF la Kanduyi ziligonga mwamba na alipoona siku za kuripoti zinaisha aliamua kutembea kwa miguu kutoka Musikoma hadi Shule ya Wavulana ya  Ndivisi eneobunge la Webuye Mashariki.

mamangu huchoma Mahindi na nina Ndugu zangu ambao pia wanamtegemea, alijaribu kutafuta karo lakini njia zote zikashindikana,” Owino alisema.

Owino ambaye alikuwa tu na barua na sare ya shule ya msingi na patipati zilizochanika  anatoa wito kwa wahisani akiwemo mbunge wa Kanduyi John Makali na gavana wa kaunti ya Bungoma Keneth Lusaka kumsadida ili alipe karo na kumuwezesha kutimiza ndoto yake ya kuwa daktari.

“Mbunge Wangu Joh Makali naomba unihurumie unisaidie hata Basari niendelee na masomo yangu nikuwe Daktar.” Alisema

Aemuomba wakilishi wadi eno hilo Bw Makabichi pia kumsaidia afanikishe donto zake.

Mwalimu mkuu wa shule ya Wavulana ya  Ndivisi Martin Wachiye alimpokea mwanafunzi huyo lakini anatoa wito kwa wahisani kujitokeza na kumlipia karo ili atimize ndoto yake.