Saturday, 19 October 2024

Wanyama ataka kiwanda cha Maziwa kimalewa Kufufuliwa


 Mwanahararakati wa sasa kaunti ya Bungoma John Wanyama anataka serikali ya kaunti ya Bungoma kufufua kiwanda cha maziwa cha kimalewa.

Akizungumza akiwa wadi ya Mukuyuni eneo binge la kabuchai kwenye hafla  moja ya mazishi Wanyama amelaumu viongozi waliochaguliwa kwa kuwasahau  wananchi na kuacha viwanda muhimu kaunti ya Bungo  kuanguka kikiwemo cha maziwa cha Kimalewa.

"Hii Bungoma  viwanda vyote vimeanguka, hiki cha maziwa pia hakuna kiongozi anakishughulikia, naomba gavana Lusaka na na spika Moses wetangula  wasaidie watu wetu," Wanyama alisema.

Ameelezea kusikitishwa kwake na pia kiwanda cha maziwa cha webuye ambacho hakijaanza kufanya kazi licha ya serikali kutumia pesa nyingi  kukijenga

Wanyama ambaye ametangaza nia ya kuwania useneta mwaka wa 2027 anataka wakaazi wa kaunti ya Bungoma kumchagua viongozi watakaotetea maslahi yao.