Monday, 10 June 2024

PALANG'A AONYA WABUNGE DHIDI YA MSWAADA WA FEDHA

Huku waziri wa fedha Njuguna Ndung’u  akitarajiwa kusoma makadirio ya bajeti ya mwaka 2024/2025,Mwakilishi wadi ya Olkaria Peter Palang’a anataka wabunge kuondoa ushuru kwa bidhaa muhimu.



Akizungumza akiwa Bokoli kaunti ya Bungoma  Palan’ga amesema  serikal inawadhulumu wananchi kwa kuongeza ushuru wa bidhaa muhimu licha ya Rais Willia Ruto kuahidi kwamba angewasaidia kupunguza ghrama ya maisha

“Kuna watu wanamdanganya Rais na kumshauri apandishe ushuru wa bidhaa muhimu, tunamuomba akumbuke ahadi alizotoa kwa mwananchi wa kawaida wakati wa kampeni,” Palang’a alisema.

Palang’a ambaye amekuwa mwakilishi wadi wa Olkaria kwa miaka 20 anataka wabunge kuangazia mswada wa fedha wa Mwaka wa 2024/2025  akisema watakuwa na maswali ya kuwajibu wakenya waliowachagua.

“Wabunge wetu tunawasihi muangazie kilio cha wakenya, wanaumia na gharama ya ju ya maisha na kuongeza ushuru mwingine kutaendelea kuwaumiza zaidi,” aliongeza

Palanga alisema haya kwenye hafla ya kufuzu kwa wanafunzi wa masomo ya teknolojia kutoka eneobunge la Webuye Magharibi.

Kwenye mradi huo zaidi ya wanafunzi mia tano wamepokea mafunzo ya  teknolojia yanayofadhiliwa na Peter Palang’a huku akitaka vijana zaidi kujitokeza ili wanufaike na masomo hayo .



No comments:

Post a Comment