Mwanaharakati wa siasa John Wanyama anataka wakaazi wa kaunti ya Bungoma kuchagua viongozi walio na uwezo wa kuwawakilisha vyema Bungeni.
Akizungumza katika hafla moja ya mazishi Malaha Webuye Magharibi Wanyama amewasuta Wabunge na maseneta kwa kushindwa kumtetea mwananchi wa kawaida na badala yake kuwakilisha tumbo zao Bungeni.
"Munaona gharama ya maisha inapanda kwa sababu ya wabunge tuliowachagua, wanaruhusu serikali kupandisha bei ya bidhaa muhimu na kumnyanyasa mwananchi", Wanyama alisema.
Wanyama ambaye pia ametangaza azma yake ya kuwania kiti cha useneta kaunti ya Bungoma anasema seneta wa sawa David Wakoli hana makali ya kumtetea mkaazi wabungoma katika bunge la seneti.
Anataka wakaazi kumchagua kwenye uchaguzi mkuu ujao akisema seneta wa sasa ameshindwa kutekeleza wajibu wake.
Ameongza kiwa kaunti ya Bungoma kwa sasa Haina mwangalizi wa serikali jambo ambalo linaruhusu ufisadi kuendelea
No comments:
Post a Comment