Serikali ya kaunti ungoma imedhibitisha kwamba watu wawili wameaga dunia kufuatia mkasa wa jengo ambalo liliporomoka walipokuwa wakijaribu kuokota vyuma kuuu eneo la kanduyi.
Kwenye ujumbe wake kwa vyombo vya habari gavana wa kaunt ya
Bungoma Keneth Lusaka anasema wiwili hao
waliokolewa na maafisa wa mikasa kaunti ya Bungoma na waliaga walipokuwa
wakipokea matibabu.
Ripoti kutoka hospitalini inaashiria kwamba wawili hao
waliaga baada ya kupoteza damu nyingi.
Gavana Lusaka ameagiza uchunguzi kufanywa na kubaini kwanini jengo
hilo halikuangushwa jinsi ilivyokuwa imeratibiwa.
Ameongeza kuwa serikali ya kaunti itawajibikia mazishi ya
wawili hao.
No comments:
Post a Comment