Friday, 10 May 2024

WAT 2 WAAGA BAADA YA KUOKOLEWA KUTOKA JENGO LA KANDUYI


Serikali ya kaunti ungoma imedhibitisha kwamba watu wawili wameaga dunia kufuatia mkasa wa jengo ambalo liliporomoka walipokuwa wakijaribu kuokota vyuma kuuu eneo la kanduyi.

Kwenye ujumbe wake kwa vyombo vya habari gavana wa kaunt ya Bungoma Keneth Lusaka anasema  wiwili hao waliokolewa na maafisa wa mikasa kaunti ya Bungoma na waliaga walipokuwa wakipokea matibabu.

Ripoti kutoka hospitalini inaashiria kwamba wawili hao waliaga baada ya kupoteza damu nyingi.

Gavana Lusaka ameagiza uchunguzi kufanywa na kubaini kwanini jengo hilo halikuangushwa jinsi ilivyokuwa imeratibiwa.

Ameongeza kuwa serikali ya kaunti itawajibikia mazishi ya wawili hao.

 

No comments:

Post a Comment