Tuesday, 7 May 2024

KITENDAWILI CHA WANGAMATI’S

Familia ya aliyekuwa gavana wa kaunti ya Bungoma Wycliffe wangamati inakadiria hasara baada      ya jumba 

la dhamani ya mamilioni ya pesa kubomolewa kufuatia ujenzi wa uwanja wa Masinde Muliro unaoendelea.

Ujenzi huo unalenga kukamilika kabla ya sherehe za madararka huku serikali ya kaunti ya Bungoma ikibomoa majengo yanayokaribia uwanja wa masinde Muliro.


Familia ya Wangamati Ikiongozwa na aliyekuwa gavana Wyclife Wangamati imekashifu  hatua hiyo ikisema ilipata ardhi hiyo kisheria.

Patrick wangamati ambaye ni mmiliki wa jengoi hilo anasema kuwa alifuata sheria mwaka wa 1968 kupata ardhi hiyo kwa ajili ya Biashara.

“Mimi sio mwizi wa Mashamba, nilifuata sheria na serikali ikanipa ardhi hii na nimekuwa nikiendeleza bisharazangu mahali hapa, nashangaa kwanini wanabomoa nyumba yangu,” Mzee wangamati alisema.

Ubomozi huo umeibua hisia mseto kutoka kwa wafuasi wa aliyekuwa gavana Wycliffe  Wangamati wakimtuhumu gavana Keneth Lusaka na spika Moses Wetangula kwa kumulenga  kisiasa.

Hata hivyo mradi wa ujenzi wa uwanja wa Masinde Muliro ulianzishwa na aliyekuwa gavana Wycliffe Wangamata alipokuwa uongozini. Wakati uo huo alianzisha ujenzi wa barabara kuu mjini Bungoma maarufu kama (dual carriage).

Wangamati alinukuliwa akisema kuwa wale wote waliojenga kwenye ardhi ya serikali waondoe majenge  hayo ili kuruhusu ujenzi wa miradi hiyo miwili mikuu la sivyo serikali itekeleze ubomozi huo.

Wapinzani wake wanadai kuwa alinuia kutumia wadhifa wake kujilinda dhidi ya ubomozi huo.





No comments:

Post a Comment