Friday, 10 May 2024

WAHOFIWA KUAGA BAADA YA KUANGUKIWA NA JENGO KANDUYI

Vijana waliokuwa wakiokota vyuma kuukuu kwenye jengo la Wangamati wamefunikwa na vifusi ikihofiwa kwamba huenda wameaga dunia baada ya jengo hilo kuporomoka.

Miongoni mwao ni vijana wanaorandaranda mitaani waliokuwa wakiokota vyuma kutoka eneo hilo.

serikali ya kaunti ya  Bungoma ilianza ubomozi wa jengo hilo linalomilikiwa na familia ya aliyekuwa gavana wa kaunti ya Bungoma Wycliffe Wangamati.

Aliyekuwa gavana Wycliffe wangamati ameisuta serikali ya kaunti kwa utepetevu wake   ambao umepelekea maafa hayo.

kwenye mtandao wake wa kijamii wangamati na Nduguye Winston Wangamati 
wametaka serikali ya kaunti kuwajibikia maafa hayo.


shughuli za uokozi zinaendelea  huku kitengo cha kukabiliana na mikasa kaunti ya Bungoma kikiwa katika njia panda kwa kukosa vifaa vya kukabiliana na mikasa

No comments:

Post a Comment