Wakaazi zaidi ya elfu mia moja kutoka mlima elgon, kabuchai na kanduyi watanufaika na maji safi baada ya serikali ya kaunti ya Bungoma kwa ushirikiano na serikai ya Korea kuzindua mradi wa maji eneo la mlima elgon.
Mradi huo wa maji uliozinduliwa na balozi wa taifa la Korea Yeo
Sung-Jun na gavana wa kaunti ya Bungoma
Keneth Lusaka unalenga kuongeza idadi ya
wakaazi wanaopata maji safi ya matumizi.
“Huu mradi wa KOICAII utafaidi wakaazi wetu hapa Mlima Elgon
na maeneo bunge jirani kama Kabuchai na kandui na tunalenga kuzindua miradi
zaidi ya maji.” Gavana Lusaka alisema.
Balozi wa taifa la Korea amesema mradi huo umegharimu
shilingi mlioni mia sita na hivi karibuni
taifa hilo litashirikiana na serikali ya kaunti ya Bungoma kuanzisha
mraidi wa KOICA III .
Swala la maji limekuwa donda sugu kwa wakaazi wa kaunti ya
bungoma licha ya kuwa na vyanzo vingi vya maji.
No comments:
Post a Comment