Mwakilishi wadi ya Matulo Stephen
Kaiser Simiyu amepeanan basari kwa
Wanafunzi kutoka wadi yake huku
ikiwa mara ya kwanza wanafunzi wengi kunufaika na basari ikilinganishwa na
miaka ya hapo awali.
Akizungumza baada ya
kuzindua zoezi hilo katika shule mbalimbali eneo hilo,mwakilishi wa wadi ya huyo Stephen Kaiser amesema awamu ya kwanza ya
shilingi milioni mbili imetolewa katika shule mbalimbali na kuwataka wazazi
ambao hawajapokea fedha kwa sasa kuwa na subira huku hawamu ya pili ikitarajiwa
hivi karibuni.
“Niliahidi kwamba nitasaidia wanafunzi
wasiojiweza kupata masomo , kwa hivyo wale wazazi ambao hawajapata tutawapa katika awamu ya pili wasiwe na
wasiwasi,” Kaiser alisema.
Kaiser hata hivyo amewataka
wanafunzi walionufaika na fedha hizo kutia bidii masomoni mwao ili waweze
kuafikia malengo yao maishani mwao.
“hatutakubali
kumalizia pesa za umma kwa mwanafunzi anayefanya vibaya katika masomo yao,
musipoweka bidii mutakuwa munaharibi masiha yenu ya mbeleni,” alisistiza
Baadhi ya shule
zilizonufaika ni kama vile, Shule ya wasichana ya Matulo, shule ya upili ya
malaha, St Mathews na zingine.


No comments:
Post a Comment