Thursday, 6 July 2023

SARATANI SIO MWISHO WA MAFANIKIO- DKT. ESTHER NDARE

 Waathiriwa wa ugonjwa wa Saratani kaunti ya Bungoma wameanzisha miradi ya kuwainua kiuchumi ili kukabiliana na changamoto za kifedha wanazokumbana nazo

Mkurugenzi wa shirika la Better World Daktari Esther Ndare ambaye pia ni mwathiriwa amesema wamechukua hatua hii baada ya jamaa zao kuwatenga kutokana na gharama ya juu ya matibabu,
wengi wetu hawana pesa za matibabu  huku wengine wakiwa wamebakia bila pesa zozote zabaada ya kupata matibabu, miradi kama ya kuku, kushona na kilimo itatufaidi,” alisema
Hata hivyo wametoa wito kwa serikali ya kaunti kuimarisha huduma za matibabu za matibabu ya saratani ili kupunguza mzigo wa kutafuta matibabu hayo Eldoret.
“Ikiwa serikali itaanza kutoa matibab

KUSHOTO DK ESTHER NDARE NA WAATHIRIWA WA SARATANI

u ya saratani hapa Bungoma tutapunguza  safari za kuenda eldoret kutafuta matibabu.” Bi Ndare alisisitiza.

Anasema shirika la  Better World hupenan pesa za chakula na mahali pa kulala kwa wathiriwa huku akitaka wahisani zaidi kujitokeza na kuwasaidia.
Waathirwa wa saratani waliopona wanasema wamepitia hali ngumu ya Maisha wakitaka wale ambao hawajajua hali zao kutembelea vituo vya afya na kupimwa.


No comments:

Post a Comment