Saturday, 19 October 2024

Wanyama ataka kiwanda cha Maziwa kimalewa Kufufuliwa


 Mwanahararakati wa sasa kaunti ya Bungoma John Wanyama anataka serikali ya kaunti ya Bungoma kufufua kiwanda cha maziwa cha kimalewa.

Akizungumza akiwa wadi ya Mukuyuni eneo binge la kabuchai kwenye hafla  moja ya mazishi Wanyama amelaumu viongozi waliochaguliwa kwa kuwasahau  wananchi na kuacha viwanda muhimu kaunti ya Bungo  kuanguka kikiwemo cha maziwa cha Kimalewa.

"Hii Bungoma  viwanda vyote vimeanguka, hiki cha maziwa pia hakuna kiongozi anakishughulikia, naomba gavana Lusaka na na spika Moses wetangula  wasaidie watu wetu," Wanyama alisema.

Ameelezea kusikitishwa kwake na pia kiwanda cha maziwa cha webuye ambacho hakijaanza kufanya kazi licha ya serikali kutumia pesa nyingi  kukijenga

Wanyama ambaye ametangaza nia ya kuwania useneta mwaka wa 2027 anataka wakaazi wa kaunti ya Bungoma kumchagua viongozi watakaotetea maslahi yao.


Monday, 10 June 2024

PALANG'A AONYA WABUNGE DHIDI YA MSWAADA WA FEDHA

Huku waziri wa fedha Njuguna Ndung’u  akitarajiwa kusoma makadirio ya bajeti ya mwaka 2024/2025,Mwakilishi wadi ya Olkaria Peter Palang’a anataka wabunge kuondoa ushuru kwa bidhaa muhimu.



Akizungumza akiwa Bokoli kaunti ya Bungoma  Palan’ga amesema  serikal inawadhulumu wananchi kwa kuongeza ushuru wa bidhaa muhimu licha ya Rais Willia Ruto kuahidi kwamba angewasaidia kupunguza ghrama ya maisha

“Kuna watu wanamdanganya Rais na kumshauri apandishe ushuru wa bidhaa muhimu, tunamuomba akumbuke ahadi alizotoa kwa mwananchi wa kawaida wakati wa kampeni,” Palang’a alisema.

Palang’a ambaye amekuwa mwakilishi wadi wa Olkaria kwa miaka 20 anataka wabunge kuangazia mswada wa fedha wa Mwaka wa 2024/2025  akisema watakuwa na maswali ya kuwajibu wakenya waliowachagua.

“Wabunge wetu tunawasihi muangazie kilio cha wakenya, wanaumia na gharama ya ju ya maisha na kuongeza ushuru mwingine kutaendelea kuwaumiza zaidi,” aliongeza

Palanga alisema haya kwenye hafla ya kufuzu kwa wanafunzi wa masomo ya teknolojia kutoka eneobunge la Webuye Magharibi.

Kwenye mradi huo zaidi ya wanafunzi mia tano wamepokea mafunzo ya  teknolojia yanayofadhiliwa na Peter Palang’a huku akitaka vijana zaidi kujitokeza ili wanufaike na masomo hayo .



BUNGOMA HAINA SENETA MCHAPAKAZI-WANYAMA ADAI

 Mwanaharakati wa siasa John Wanyama anataka wakaazi wa kaunti ya Bungoma kuchagua viongozi walio na uwezo wa kuwawakilisha vyema Bungeni.



Akizungumza katika hafla moja ya mazishi Malaha Webuye Magharibi Wanyama amewasuta Wabunge na maseneta kwa kushindwa kumtetea mwananchi wa kawaida na badala yake kuwakilisha tumbo zao Bungeni.

"Munaona gharama ya maisha inapanda kwa sababu ya wabunge tuliowachagua, wanaruhusu serikali kupandisha bei ya bidhaa muhimu na kumnyanyasa mwananchi", Wanyama alisema.

Wanyama ambaye pia ametangaza azma yake ya kuwania kiti cha useneta kaunti ya Bungoma anasema seneta wa sawa David Wakoli hana makali ya kumtetea mkaazi wabungoma katika bunge la seneti.

Anataka wakaazi kumchagua kwenye uchaguzi mkuu ujao akisema seneta wa sasa ameshindwa kutekeleza wajibu wake.

Ameongza kiwa kaunti ya Bungoma kwa sasa Haina mwangalizi wa serikali jambo ambalo linaruhusu ufisadi kuendelea

Friday, 10 May 2024

WAT 2 WAAGA BAADA YA KUOKOLEWA KUTOKA JENGO LA KANDUYI


Serikali ya kaunti ungoma imedhibitisha kwamba watu wawili wameaga dunia kufuatia mkasa wa jengo ambalo liliporomoka walipokuwa wakijaribu kuokota vyuma kuuu eneo la kanduyi.

Kwenye ujumbe wake kwa vyombo vya habari gavana wa kaunt ya Bungoma Keneth Lusaka anasema  wiwili hao waliokolewa na maafisa wa mikasa kaunti ya Bungoma na waliaga walipokuwa wakipokea matibabu.

Ripoti kutoka hospitalini inaashiria kwamba wawili hao waliaga baada ya kupoteza damu nyingi.

Gavana Lusaka ameagiza uchunguzi kufanywa na kubaini kwanini jengo hilo halikuangushwa jinsi ilivyokuwa imeratibiwa.

Ameongeza kuwa serikali ya kaunti itawajibikia mazishi ya wawili hao.

 

VUGUVUGU LA MAZINGIRA CONSERVATION LAPANDA MICHE YA MITI 3000 WEBUYE

Kikundi cha kulinda mazingira cha “Mazingira Conservation” kiomeongoza zoezi la upanzi wa miti eneo bunge la Webuye magharibi huku wakipanda zaidi ya miche elfu tatu katika shule eneo hilo.



Mwenyekiti wake Edward Kimakwa anasme kuwa wamekuwa wakiendeleza zoezi la upanzi wa miti katika shule na makanisa eneo hilo na agizo la raisi la kupanda miti linawiana na ajenda ya vuguvugu hilo.

Kimakwa amewahimiza wakaazi wa kaunti ya Bungoma kupanda miti kwa wingi akiwataka kupunguza ukataji wa miti kiholela.

“Tumekata miti  kwa wingi na huenda kizazi kijacho kikaathirika, kwa sasa hata kuna aina fulani za wanyama na ndege ambao wameadimika kutokana na uharibifu wa mazingira,” Kimakwa alisema

Mwanamazingira huyo ametoa wito kwa viongozi waliochaguliwa kutenga pesa na kununua miche ambayo inaweza kupeanwa kwa wakulima bure ili wapanda.

Ametaka pia serikali ya kitaifa kutobagua waathiriwa wa mvua kaunti ya Bungoma wakati wa kupeana msaada.

“Tuna wakaazi wengi kaunti yetu ya Bungoma walioathirika na mvua inayoendelea, baadhi yao nyumba zimeanguka na wengine mimea yao imeharibiwa na mafuriko, naomba  rais William Ruto  ahakikisha watu wetu pia wanafidiwa kwa hasara waliopata,” Kimakwa alisisitiza.

Kauli yake imeungwa mkono na chifu wa kata ya Miendo Carolye Lwiki  na mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya miendo Christine makamu waliowataka wakaazi wa eneo hilo kutumia mvua inayonyesha kwa sasa kupanda miti kwa wingi.

Nao baadhi ya vijana wa kikundi hicho wakiongozwa na katibu wao Nickson Machani wamewataka vijana wenzao kukumbatia upanzi wa miti wakisema huenda ikawanufaisha siku za usoni.

“Vijana wengi hukata tu miti lakini hawakumbuki kupanda, ndio sababu kupitia kwa mfadhili wetu Edward Kimakwa tunapanda miti ili kulinda kizazi kijacho,” Machani alisema


Haya yanajiri wakati ambao taifa la Kenya linashuhudia mvua nyingi huku mamia ya watu wakiathirika  na wengine kuaga dunia.

 

WAHOFIWA KUAGA BAADA YA KUANGUKIWA NA JENGO KANDUYI

Vijana waliokuwa wakiokota vyuma kuukuu kwenye jengo la Wangamati wamefunikwa na vifusi ikihofiwa kwamba huenda wameaga dunia baada ya jengo hilo kuporomoka.

Miongoni mwao ni vijana wanaorandaranda mitaani waliokuwa wakiokota vyuma kutoka eneo hilo.

serikali ya kaunti ya  Bungoma ilianza ubomozi wa jengo hilo linalomilikiwa na familia ya aliyekuwa gavana wa kaunti ya Bungoma Wycliffe Wangamati.

Aliyekuwa gavana Wycliffe wangamati ameisuta serikali ya kaunti kwa utepetevu wake   ambao umepelekea maafa hayo.

kwenye mtandao wake wa kijamii wangamati na Nduguye Winston Wangamati 
wametaka serikali ya kaunti kuwajibikia maafa hayo.


shughuli za uokozi zinaendelea  huku kitengo cha kukabiliana na mikasa kaunti ya Bungoma kikiwa katika njia panda kwa kukosa vifaa vya kukabiliana na mikasa

Thursday, 9 May 2024

AFUENI YA MAJI SAFI MLIMA ELGON

Wakaazi zaidi ya elfu mia moja kutoka mlima elgon, kabuchai na kanduyi  watanufaika na maji safi  baada ya serikali ya kaunti ya Bungoma kwa ushirikiano na  serikai ya Korea kuzindua mradi wa maji eneo la  mlima elgon.



Mradi huo wa maji uliozinduliwa na balozi wa taifa la Korea Yeo Sung-Jun  na gavana wa kaunti ya Bungoma Keneth Lusaka  unalenga kuongeza idadi ya wakaazi wanaopata maji safi ya matumizi.

“Huu mradi wa KOICAII utafaidi wakaazi wetu hapa Mlima Elgon na maeneo bunge jirani kama Kabuchai na kandui na tunalenga kuzindua miradi zaidi ya maji.” Gavana Lusaka alisema.

Balozi wa taifa la Korea amesema mradi huo umegharimu shilingi mlioni mia sita na hivi karibuni  taifa hilo litashirikiana na serikali ya kaunti ya Bungoma kuanzisha mraidi wa KOICA III .



Swala la maji limekuwa donda sugu kwa wakaazi wa kaunti ya bungoma licha ya kuwa na vyanzo vingi vya maji.