Mwaniaji wa kiti Cha useneta kaunti ya Bungoma Machacha Majembe mapangulula amesema Yuko katika nafasi Bora kumbandua seneta wa kaunti ya Bungoma Moses wetangula.
Majembe amepuuzilia mbali wale wanosema kuwa naibu gavana Charlis Ngome awanie useneta kupitia chama Cha UDA akisema, Ngome hatawezana na Kiti hicho.
"Naambia Ngome hatawezana na hii kiti, ni Mimi tu nitambandua Wetangula na namuomba awe tayari kukubaliana na matokeo." Alisema.
Majembe ameonyesha Ari yake ya kuwania kiti Cha useneta kupitia chama Cha UDA, ushindani mkali ukitarajiwa baina yake na seneta wa Sasa Moses Wetangula

No comments:
Post a Comment