Mwakilishi wadi ya Ndivisi Martin Wanyonyi amesema kuwa yuko
katika nafasi bora kumridhi Mbunge wa sasa wa Webuye Mashariki Alfred Sambu.
| MARTIN WANYONYI (KATIKATI) AKIWA MAKUSELWA |
Akizungumza akiwa Makuselwa
katika Hafla moja ya Mazishi Wanyonyi amesema
ataleta mageuzi makubwa eneobunge la Webuye Mashariki akiwataka wakaazi
eneo hilo kumchagua katika uchaguzi mkuu ujao.
“kati ya hawa wanasiasa munaona wakitembea ni mimi pekee yangu
niko na rekodi nzuri ya utendakazi, wengine wao wamejihusisha na ukora na
ulaghai, sasa wanataka kutuletea ufisadi hapa Webuye East, wakija muwapuuzilie
mbali,” wanyonyi alisema.
Wanyonyi ameongeza kuwa akiwa mbunge atahakikisha swala la kupeana
basari, kandarasi na ajira litafanywa kwa usawa bila ufisadi.
“Mmejionea vile nimenyorosha wadi ya Ndivisi kwa miaka mitano
pekee, mukinipa ubunge hamtajuta kunipa nafasi hiyo,” aliongeza.
Ameongeza kuwa atapigania
haki za wakaazi likiwemo swala la mlima chetambe
chetambe ili wakaaazi wasifurushe katika mashamba yao.
Upinzanimkali unatarajiwa katika uchaguzi mkuu ujao kiti cha webuye mashariki kikivutia wanasiasa wengi akiwemo Caro Buyela na Dkt Iyaya wanjala
No comments:
Post a Comment