Friday, 12 November 2021

RAILA AJITENGE NA VURUGU ZA NYANZA NA AHUBIRI AMANI KWA WAFUASI WAKE

Viongozi wa kidini kaunti ya Bungoma wanamtaka kinara wa chama cha ODM Raila Odinga kujitokeza na kuelimisha wakaazi wa Nyanza kuhusiana na umuhimu wa uwiano na utangamano msimu huu wa siasa.

Hii inakuja Siku chache  tu baada ya msafara wa naibu rais William Ruto kushambuliwa  kwa mawe na baadhi ya vijana katika eneo la Kondele kaunti ya Kisumu.

Maaskofu  hao  David Walukhu na Hamphry Wanyama  wamejitokeza na kukashifu vurugu hizo na kutaka viongozi wa kisiasa kukoma kuwatumia vijana vibaya wakisema kitendo hicho huenda kikarejesha taifa hili kwenye michafuko ya kisiasa.

“Itakuwa vyema ikiwa kinara wa ODM atajitokeza wazi na kujitenga na vurugu hizo na pia ashauri wakaazi wa Kisumu kudumisha amani jinsi tulivyo ona wakenya wengine walivyofanya katika mikutn tofauti ya kisiasa inayofanywa na wanasiasa nchini,” akofu Wanyama alisema.

BISHOP HAMPHRY WANYAMA-JESUS TO ALL NATIONS CHURCH


Askofu walukhu naye ametaka wanasiasa pia kuhubiri amani kabla ya uchaguzi mkuu ujao akisema mungu mwenyewe atachagua mtu atakayemridhi rais Uhuru Kenyatta.

“Hatutaki vurugu za mwaka wa 2007 zirejelewe tena, tunawaomba wanasiasa hasa walewanaowania uraise wahubiri amanai, hatutaruhusu mwenendo kama uliokuwa Kondele kuendelea nchini wakti ambapo makovu ya vurugu za mwaka wa 2007 hayajapona,” Akofu walukhu alisema.

BISHOP DAVID WALUKHU-MWENYEKITI WA WAHUBIRI WEBUYE WEST SUBCOUNTY


Viongozi hao hata hivyo wamewahimiza vijana kukoma kutumiwa vibaya na wanasiasa hao na badala yake kujihusisha na maswala muhimu ya taifa.





No comments:

Post a Comment