Wednesday, 3 November 2021

STEVE SONKO APIGA JEKI AKINANA MAMA NA MAKANISA MATULO

 Wajane 150 wamenufaika na msaada wa shilingi 40,000/= kutoka kwa mwaniaji wa kiti cha  mwakilishi wadi ya Matulo Steve Simiyu ili kufanikisha miradi katika kikundi Chao.

MWAKILISHI WA WAKFU WA STEV KAISER AKIZUNGUMZA NA WAJANE
Akizungumza baada ya kutoa msaada huo kwa kikundi Cha Balekhwa self Helf Group  Steve maarufu kama Sonko amesema kuwa huu ni mwanzo wa wajane kunufaika na uongozi wake pindi atakapochaguliwa kuwakilisha wadi ya Matulo katika  bunge la kaunti ya Bungoma.

"Kwa muda tumekosa mtetezi wa wajane Matulo, na huu ndio wakati nawaomba mnipe nafasi ya kuwakilisha ili mufurahie uongozi Bora", Simiyu alisisitiza.

Kikundi Cha Balekhwa self help group ni mojawapo ya vikundi vya wajane wadi ya Matulo vilivyonufaika na msaada wa wakfu wa  Steven Kaiser.


Msaada wa mabati kwa kanisa Matulo

 Kando na wajane kanisa la Hope of God Matulo pia limepokea Mabati 40 kutoko kwa wakfu wa Stev Kaiser ili kukamilisha ujenzinwake.

Kiongozi wa kanisa Hilo Daniel Amunaba anasema imechukua muda mrefu kukamilisha kanisa Hilo akisema msaada kutoka kwa wakfu huo ulio chini ya Steve kaiser Simiyu utawasaidia kukamilisha jengo Hilo.

Muhubiri huyo ameongeza kuwa juhudi zao za kupata ufadhili ziligonga mwamba Hadi walipomfikia Steve sonko.

MAPEMA KABLA KUPELEKA MABATI KANISANI

Akizungumza na mwandishi wa Makala haya Steve Songo amesema analenga kutoa ufadhili wake kwa makanisa, makundi ya vijana, akina mama na  Watu binafsi ili kuinua hali ya maisha ya wakaazi wa Matulo.






No comments:

Post a Comment