![]() |
| TIMOTHY WANJALA NA MKEWE CARLYNE NEKESA HOSPITALINI WEBUYE |
Wanjala ambaye
ni mkaazi wa Bahai eneo bunge la Kimili anasema wamekuwa wakipitia hali ngumu
ili kugharamia matibabu ya mkewe
Timothy
Wanjala Simiyu ambaye pia ana ulemavu wa
macho anasema mkewe Carolyne Nekesa alilazwa
na kufanyiwa upasuwaji mkononi ili kuondoa uvimbe lakini baada ya matibabu hayo hawana njia nyingine
ya kulipia matibabu hayo wakitoa wito
kwa wahisani kuingilia kati na kuwasaidia ili warejee nyumbani.
“
Nimejaribu kutumia kadi yangu ya NHIF lakini imeshindikana baada ya usimamizi
wa hospitali ya Webuye kuniambia kuwa sijalipia kadi hiyo kwa muda wa miezi
kumi na miwili ijayo, sasa sina jinsi nitakavyolipia matibabu ya mke wangu,”
Wanjala alisema
Kwa sasa
Wanjala na mkewe wamezuliwa katika hospitali ya Webuye akisema kuzuiliwa kwake kumefanya hana jinsi ya
kutafuta pesa hizo ili amlipie mkewe
gharama za matibabu.
“Nimeshindwa
jinsi nitakavyomsadia mke wangu, mimi mwenye sina uweza wa kuona hata
nikiondoka hapa sijui nitaanzia wapi ndiposa nipate pesa hizo, naomba
munisaidie mimi na mke wangu turudi nyumbani tuangalie watoto wetu,” alisema.
Wanjala ambaye
ni baba wa watoto saba anasema tangu mkewe aanze kuugua na kusambaa kwa ugonjwa
wa Covid 19 nchini wamekuwa wakipitia
hali ngumu kukidhi mahitaji ya wanao 7
pamoja na matibabu ya mkewe.
“Sai
wanangu hawana mlezi nyumbani, naomba Mbunge wangu mpoendwa Didimus barasa na
Mca wangu au mtu anayeweza kunisadia tu nilipe hizi pesa, nikiondoka nitajua
jisni ya kujipanga,” aliomba.
Nambari ya
Timothy Wanjala 0711626847


No comments:
Post a Comment