Chama cha Ford Kenya kimeweka mikakati ya kuhakikisha kanuni na katiba ya chama hicho inazingatiwa vililvyo.
Kwenya taarifa kwa vyombo vya habari baada ya mkutano na kamati ya usimamizi wa chama hicho, Katibu mwandalizi Chris ManduMandu amesema kamati hiyo imetoa mwelekeo wa kuifanyia mabadiliko usimamizi wa makao makuu ya chama hicho mbali na kuweka mipangilio ya mkutano wa Kitaifa wanachama.
Aidha amedokeza kuwa kamati hiyo imejadili kwa undani mwongozo wa msajili wa vyama vya kisiasa ya kusuluhisha mgogoro ndani ya chama hicho na kusema tayari hatua mwafaka zimechukuliwa.
No comments:
Post a Comment