Saturday, 13 June 2020

WAZEE WATAKUSO WAGAWANYIKA KUHUSU MSEMAJI WA WALUHYA HUKU WAZIRI EUGINE WAMALWA NA GAVANA OPARANYA WAKIVUNJA SHERIA ZA KUDHIBITI KORONA

Jamii ya Watachoni imegawanyika kuhusiana na hatua ya Baraza la wazee wa jamii hiyo kujitokeza na kusema kuwa wanaunga mkono  gavana wa kaunti ya kakamega  Wycliffe Oparanya na waziri Eugine wamalwa kuwa waswemaji wa jamii ya waluhya.

SE-WEKESA- MWENYEKITI WA TAKUSO

Baada ya  kikao  cha faragani katika shule ya upili ya Lukusi na waziri Eugene Wamalwa, gavana Wycliffe Oparanya, Wycliffe Wangamati na sospiter ojamong’ wazee wa TAKUSO wakiongozwa na  Se Wekesa wamesema kuwa watmuunga mkono rais Uhuru Kenyatta na Kinara wa ODM Ralia Odinga kwenye mchakato wa BBI  kabla ya uchaguzi wa 2022, huku baadhi ya wazee wakisema kuwa hawakuhusishwa katika uamuzi huo.

“tumeamua kwa kauli Moja kuunga mkono hatua ya Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga kuunganisha taifa  na tunaomba jamii ya Tachoni, sote tuunge mkono serikali yetu.” SeWekesa alisema.

MRENGO WA WAZEE WALIOZULIWA KUINGIA MKUTANONI

Hata hivyo mugawanyiko umeshuhudiwa miongoni mwa wazee hao huku baadhi ya wazee Watachoni wakisema mkutano huo haukuhusisha viongozi wote.

Wazee hao na baadhi ya wakazi wamesema viongozi wa TAKUSO wanajitakia wenyewe na mkutano huo ulilenga kunufaisha  wachache.

Wakati uo huo mamia ya wakaazi walifurika katika shule ya upili ya Lukusi wakitarajia kupokea chakula kutoka kwa Waziri Eugene wamalwa  huku watu Kumi wakipokea  gunia la 50kg la maharagwe na mafyta Lita moja ya kupika.

WALIONUFAIKA NA CHAKULA
WALIONUFAIKA NA CHAKULA

UMATI KATIKA MKUTANO WA SIASA LIKUSI

Wazri  huyo na magavana Oparanya, Ojamong’ na gavana Wangamati waliendeleza siasa za BBI kwa kisingizia cha kugawa chakula huku wakaazi wakifurika katika uwanja wa shule ya upili ya Lukusi bila kujali Sheria za kuzua maambukizi ya Covid 19.


Wanne hao wametoa wito kwa jamii ya Tachoni kuunga mkono mrengo wa Handshek wakisema mrengo wa Tangatanga hautaweza kuwapa maendeleo.

“tunataka jamii ya Mlembe iwe serikali, na Mimi na mwenzangu Oparanya ndio tuko katika nafasi Bora ya kuwatetea serikali,” waziri wamalwa alisema.


No comments:

Post a Comment