Wednesday, 10 June 2020

BAADHI YA MADIWANI BUNGOMA WAUNGA KUBANDULIWA KWA WETANGULA

Zaidi ya  madiwani wastaafu kumi na tano kutoka kaunti ya wamejitokeza na kupongeza mageuzi yaliyofanywa katika chama cha Fordkenya hivi majuzi wakisema kuwa aliyekuwa kinara wa chama hicho Moses Wetangula  amekuwa akiwakandamiza wanachama .
Wakizungumza na wanahabri mjini Webuye madiwani hao wastaafu  wakiongozwa Patrick Manyonge na Ben Wambalaba wamesema kuwa hatua hiyo ya kubanduliwa kwa Wetangula ilistahili kwa kuwa kinara huyo amechangia viongozi wengi kugura chama hicho na kuondoka kwake huenda kukawarejesha viongozi hao.

No comments:

Post a Comment