Seneta wa kaunti ya Bungoma Moses Wetangula amepuuzilia mbali
madai ya Mbunge wa Tongaren Eseli Simiyu
kuwa mrengo wake ulichangia kuteuliwa kwa naibu Chanzela wa Chuo kikuu
cha Kibabi Prof. Dolnald Siamba.
Wetangula anasema waziri Eugine Wamalwa, Eseli Simiyu na
Mbunge wa Kanduyi Wafula Wamunyinyi hawakuhusika kwa vyovyote katika kuteuliwa
kwa Siamba akisema wanajaribu kutumia swala hilo kujinufaisha kisiasa.
“ Kama Wamalwa yuko Serikalini alikuwa anaenda kumuona Raila
kama nani? Raila odinga hayuko serikalini na hana uwezo wowote wa kumteua mtu
katika wadhifa wa taasisi za uma,” Wetangula alisema.
Wetangula amesema kuwa ni yeye aliyefanya mazungumzo na
maafisa wakuu serikalini kuhakikisha kuwa Siamba anateuliwa.
Wetangula pia amesema chama cha Ford Kenya kitawachukulia
hatua za kinidhamu Eseli, Wamunyinyi na Wangamati kwa kujaribu kufanya
mapinduzi chamani.
Hata hivyo mrengo wa Eseli umeshikilia kuwa haumtambui Wetangula
kama kinara wa chama cha Simba.

No comments:
Post a Comment